Author: Champe

  • Photo Story: CBMC African Convention

    Photo Story: CBMC African Convention

    Find the link for the CMBC African Convention article Here.

    Photos by: Joseph Gichari

    Josephndungo55@gmail.com

  • ROGERS: UNDERPROMISE AND OVERDELIVER.

    ROGERS: UNDERPROMISE AND OVERDELIVER.

    By
    Aaron Kituku
    (kaykituku@gmail.com)

    Daystar University has today held a career talk on ethical business practices in the market place. The event hosted delegates from connecting business and market place to Christ (CBMC) on what was termed as a pre-convention on the African chapter.

    The ICT theatre at the main campus was packed with curious students and staff members ready for insights about the business world, and where the latter meets Christianity and ethics. Godwin Roger, a political science graduate and a serial entrepreneur from the United States of America was the keynote speaker.

    “You don’t have to do anything you don’t want to do […] People that say ‘No’ are focused people,” Rogers said as he emphasized the need to finding your passion, talents, and gifts as you venture into business.

    Further, he emphasized that Self-awareness, Investing in knowledge, taking action, developing skills and cultivating good habits are imperative traits that individuals need to develop to stay atop the business ladder.

    “Build relationships, people are not a transaction, people are people.” Rogers clarified. Being in business for the last 20 years, this serial investor admitted to having had zero budgets on marketing. His secret, he said, was building and maintaining good relationships with people.

    “I have never failed my entire life […] failure happens when you stop moving forward.” Said Rogers in response to a question from one of the audiences about handling failure. Setting your priorities right – God, Family, Job/Business, Ministry and Fun was, according to Rogers, the recipe to a balanced.

    “Pick whoever you want to work with… and don’t discount your value.” Said Rogers in his parting shot.

    For information, click here

  • Low turnout Plagues ECD Voter Education

    Low turnout Plagues ECD Voter Education

    By Andrew E. K. Maina
    kimemia.maina@gmail.com

    Extremely low voter turnout marked both days of of the voter sensitization training held by the Electoral Commission of Daystar (ECD). the training 14th and 15th of October in Athi River and on the 14th in Valley Road Campuses of Daystar University.

    Less than 30 people showed up for the each of the two days activity in the Amphitheatre of Athi River campus, with even lower numbers said to have participated in Valley Road.

    “The turnout was really really low. But it happens.” Clifford Kabo, an ECD commissioner for Athi River Campus said at the end of the Athi training exercise. “For us, we did our part and for those that didn’t come, we will try to send them illustrations or tutorials on how to do the voting.”

    The training exercise was intended to educate student voters in the DUSA on the new voting structures for the newly introduced DUSA Congress, and how the Congress will establish an electoral college to elect the DUSA council.

    However, there seems to have been very little awareness or interest on the part of Daystar students in the process. The Training sessions were conducted by various ECD officials, with ECD Vice-Chair Faith Riungu, ECD Chief Executive Officer, Consul Simiyu, and Athi River Commissioners Kabo Clifford and Martin Mugendi present on the second day of the Athi River exercise.

    “I expected more people to come because we are learning about voting.” Nick Keyu, a Communication Studies student in Athi River said. I don’t know much about it (the voter education exercise) myself, but I would attend another one,” he added.

    The training exercise was also intended to double up as an introduction to a new electronic voting system which will be used by students to select their representatives on the DUSA Congress.

  • SIKUKUU YA MOI YAREJESHWA TENA

    SIKUKUU YA MOI YAREJESHWA TENA

    Picha kwa hisani ya: businesstoday.co.ke

    Na Gladys Sheila,
    gladyshila52@gmail.com

    Katibu wa baraza la mawaziri katika wizara ya mambo ya ndani na uratibu wa serikali ya kitaifa Daktari Fred Matiang’i alitoa taarifa siku ya Jumanne na kuidhinisha sikukuu ya Moi kama sikukuu ya kitaifa.

    Hii ni baada ya uamuzi wa mahakama. Mnamo mwaka wa 2010, sikukuu ya Moi iliondolewa katika orodha ya sikukuu za kimataifa wakati katiba mpya ilizinduliwa rasmi. Mwezi wa Novemba mwaka wa 2017, jaji wa mahakama kuu alipinga uamuzi huo kwa kusema kuwa ni jambo ambalo linakiuka sheria. Mojawapo ya sababu ilikuwa kuwa sikukuu ya Moi haikuwa ya kuadhimisha wananchi au ufanisi wa nchi, bali mtu mmoja.

    “Kulingana na sheria kuhusu Sikukuu (Sura ya 110, Sheria za Kenya) na uamuzi wa mahakama katika Kesi ya Kikatiba Nambari 292 ya 2017, ninatangaza kuwa Oktoba 10, 2019, itakuwa sikukuu ya kitaifa,” Waziri Fred Matiang’i akasema.

    Hata hivyo, Wakenya wengi walikuwa na njia anuwai za kusherehekea siku hiyo. Wengine waliendeleza biashara zao kama kawaida, wengine wakisafiri kukutana na jamaa na familia zao na wengine wakapumzika kutoka kazini.

    Liliofanya sikukuu hii iwe ya kipekee ni kuwa wakenya wengi walitumia muda huu kuwatembelea na kuwapa msaada watoto katika nyumba za mayatima, wajane, wazee waliotengwa na familia zao, walemavu na wengineo kama ishara ya upendo.

    Hali kadhalika, wakenya wengine walikuwa na msimamo tofauti kuhusu maadhinisho ya sikukuu hiyo huku wakifananisha kipindi cha uongozi wa Mheshimiwa Moi kama dikteta.

    Picha kwa hisani ya: Nairobinews.nation.co.ke
  • MCHUANO WA KUKATA NA SHOKA

    MCHUANO WA KUKATA NA SHOKA

    Na: Dorothy Waweru
    dorothywaweru161706@daystar.ac.ke

    Picha: Wachezaji wakijikakamua uwanjani

    Sikukuu ya Moi chuoni Daystar ilisherehekewa kwa mbwembwe, vifijo na nderemo kwani katika uga wa “Santiago Barna Betheli” kama unavyojulikana na wacheza kandanda wengi, mchuano mkubwa ulikuwa ukiendelea. Mchuano huo uliandaliwa na wanafunzi wacheza kandanda ikiwemo; Walter Nalwa, Nicholas Atulo Snr, Cedrick na Dadiseh Olwaga ambao walinuia kujiburudisha katika mchezo huo wa miguu.

    Mchuano huo ulijumuisha timu sita zikiwemo: Blueboys, Rawa, Buffoons, Bomboclats, DCF handball na Fimbu. Timu hizi zilimenyana vilivyo ili kushinda zawadi murwa ambayo ilikuwa ni mbuzi mzima. Timu za Buffoons na Rawa ndizo zilifungua uga huo ambao ulikuwa na utelezi kufuatia mvua kubwa iliyokuwa imenyesha usiku wote.

    Timu ya Buffoons ilijikakamua katika dakika za kwanza huku Caleb Msando akiifungia timu hiyo bao la kwanza naye Nicholas Atulo Snr akifunga bao lao la pili. Timu ya Rawa ilijikakamua katika kipindi cha lala salama ambapo John Lemaiyan aliifungia Rawa bao lao la kwanza. Kitengo hicho cha kwanza cha mchezo kilipotamatika, Buffoons walikuwa wamefunga mabao mawili kwa moja.

    Mashabiki wa timu ya Buffoons walijaa uwanjani wakiimba nyimbo za ushindi kwani timu hiyo ingemchinja mbuzi kama zawadi ya ufanisi wao iwapo wangewashinda wenzao kwenye semifinali. Baada ya dakika chache za mapumziko, timu ya DCF handball ilijitosa uwanjani kumenyana na wachezaji wa timu ya Fimbu. Uzoefu mkuu katika mpira wa mikono wa timu ya DCF handball ulionekana kuwapa mkono uwanjani. Hata hivyo baada ya dakika kumi na tano Wallace kutoka timu ya Fimbu alifunga bao la kwanza. Baada ya dakika zingine tano, DCF handball ilisawazisha kupitia mchezaji Ephantus.

    Baada ya nusu wakati wa mchezo huo, timu ya Fimbu ilifunga bao lingine ambalo liliwawezesha kuibuka washindi katika kitengo hicho kwa mabao mawili kwa moja. Timu ya Blueboys vilevile ilichuana na timu ya Rawa huku wakifunga bao lao la kwanza ambalo lilikuwa la pekee katika mchezo huo hivi basi kuibuka washindi dhidi ya Rawa.

    Hata ingawa jua lilikuwa mtikati, wachezaji wa Bomboclat waliingia ugani kumenyana na DCF handball. Yasemekana kuwa wachezaji wa Bomboclat walikuwa wamekesha wakijitayarisha kwa mchuano huo wa kipekee. Katika dakika za kwanza, Bomboclat ilifunga bao lao la kwanza na baadaye kufunga la pili. DCF handball ilijizolea nunge hivi basi Bomboclat kuibuka washindi.

    Isitoshe, kabla ya semi fainali, Bomboclat ilichuana na Fimbu na wakailaza Fimbu bao moja kwa nunge. Timu zilizofuzu kwenye semi fainali ni Fimbu, Buffoons, Bomboclat na Blueboys. Mechi ya kwanza katika semi fainali ilikuwa kati ya Buffoons na Fimbu. Buffoons walilazwa bao moja la kufunga virago baada ya kucheza kwa ukakamavu mwingi sana.

    Nyuso za wachezaji wa timu ya Buffoons zilijaa simanzi kwani mbuzi alikuwa amewakwepa. Lisilobudi hubidi, Buffoons walidondolewa kwenye mchuano wakabaki kuwa mashabiki tu. “Ni uchungu sana mama kubeba mimba tumboni kwa miezi tisa halafu anampoteza mwana wake. Nasikitika sana kuwa tumeshindwa,” Duncan Olile, kipa wa timu ya Buffoons alisema.

    Timu za Bomboclat na Blueboys zilichuana kwenye mchezo wa pili katika semi fainali huku Bomboclat ikiibuka mshindi baada ya kuilaza Blueboys mabao mawili kwa nunge. Washindi wa semi fainali walikuwa Bomboclat na Fimbu. Wakati ukiwa saa kumi na mbili kamili, mchuano kati ya timu hizi mbili ulianza huku Bomboclat ikifunga mabao mawili mida ya dakika za kumi na tano za kwanza. Japo Fimbu iling’ang’ana kiudi na uvumba kujizolea angalau bao moja, jitihada zao hazikuzaa matunda kwani katika kipindi cha pili cha mchezo huo, Bomboclat ilifunga bao lingine. Bomboclat wakafunga mabao matatu kwa nunge.

    Mbwembwe na shamrashamra zilijaa uwanjani wakati ambapo wachezaji wa Bomboclat walipokabidhiwa mbuzi wao. Wachezaji waliachwa ugani wakisherehekea ushindi wao huku mashabiki wakiungana nao kushangilia ushindi wao.

  • KIVUKIO CHA KIFO

    KIVUKIO CHA KIFO

    Na: Dorothy Waweru
    dorothywaweru161706@daystar.ac.ke

    Picha kwa hisani ya: The Star

    Ni afueni kwa wakenya wote na haswa familia yake Bi. Mariam Kighenda kwa kutolewa katika hindi la Victoria.

    Shughuli hii iliyochukua siku kumi na tatu, imezifanya nyoyo nyingi sasa kupata na utulivu. Aila ya Bi. Mariam sasa inauhuru wa kuzipumzisha mili ya wapenda wao ambao wamesumbuka usiku kucha. Japo bado uchungu upo, tunamwomba Mwenyezi Mungu aweze kuilaza roho zao pahala pema peponi.

    Hata hivyo, Shirika la Kenya Ferry limekabiliwa na mashtaka chungu nzima kufuatia ajali iliyotokea katika kivuko cha Likoni. Ajali hiyo ilihusisha kutumbukia kwa gari moja kwenye bahari hindi mnamo Septemba ishirini na tisa mida ya saa kumi na mbili. Gari hilo lilikuwa na abiria wawili, Bi. Mariam Kighenda na mwanawe Amanda Mutheu.

    Yasemekana wawili hawa walikuwa wametoka kuzuru shamba katika kaunti ya Kwale na walikuwa wakirejea nyumbani walipopatana na kifo chao.
    Matukio yaliyojiri baadaye yanaashiria utepetevu mkuu wa shirika la Kenya Ferry katika kutekeleza majukumu yao ya kuhakikisha usalama wa wasafiri.

    Baada ya ajali hiyo kutokea siku ya Jumatatu tarehe thelathini Septemba, Kenya Ferry kupitia mtandao wa kijamii wa twitter ilitangaza kuwa watahakikisha kuna meli nne katika kivukio cha Likoni.

    Wakenya kupitia mtandao huo walituma jumbe zilizosheheni kughadhabishwa kwa usemi wa Kenya Ferry kwani la muhimu lilikuwa kuomba msamaha kwa familia ya walioadhirika badala ya kuwaambia wananchi kuwa feri nne zitatutumika kuwasafirisha abiria hapo likoni.

    Ni jambo la kukereketa maini kugundua kwamba shirika la feri halina mikakati bomba inayowahakikishia abiria usalama wao hasa wakati kuna tukio kama hilo linalohatarisha maisha yao.

    Uchunguzi ambao unaendelea kufanywa umebaini kwamba shirika la feri la humu nchini halina wapiga mbizi ambao wanasafiri katika feri mchana na usiku bali wanawategemea wapiga mbizi katika shirika la Kenya Ports Authority na jeshi la baharini humu nchini.

    Uhai wa mama Amanda na mwanawe haungekatizwa ghafla iwapo shirika la Kenya Ferry lingekuwa na wapiga mbizi katika chombo hicho wakati wa mkasa huo. Wapiga mbizi wangelikuwepo wangefanya hima kuwaokoa abiria hawa punde tu gari lao lilipoanza kuzama.

    Msemaji wa serikali Col Rtd, Cyrus Oguna alipokuwa akitoa taarifa aliwaambia wanahabari kuwa gari lilichukua chini ya dakika moja unusu kuzama kwa hivyo kulikuwa na muda tosha wa kuwaokoa wasafiri hawa.

    Sababu za kucheleweshwa kwa kutolewa kwa miili ya walioaga ni kuwa kuna meli zinazopita baharini kupitia bandari ya Mombasa kufanya biashara ambayo inailetea kaunti ya Mombasa fedha nyingi. Tunaelewa kwamba tukikatiza usafiri wa meli baharini uchumi wa Mombasa utaadhirika pakubwa.

    Sababu ya pili ni giza kali ambayo imeshuhudiwa baharini hivyo wapiga mbizi wanatatizika sana. Tatu ni mawimbi makali yanayovuma baharini hivyo shughuli za uokoaji zinagonga mwamba wakati huo hadi mawimbi yatulie. Lakini ile sababu muhimu zaidi ni kuhakikisha kuwa usalama wa wapiga mbizi na wale wote wanaohusika katika shughuli za uokoaji unadumishwa,” haya yalikuwa maoni ya msemaji wa serikali Col Rtd.Cyrus Oguna.

    Shirika la Kenya Ferry limeshuhudia visa kama hivi vya ajali bali ni hatua chache sasa zimechukuliwa kuimarisha utendakazi wao. Wasafiri hawana uhakika wa usalama wao kwani janga kama hili linaweza kutokea bila usaidizi wowote. Ni bayana kuwa uwepo wa kuwa tayari kukabiliana na mikasa ya baharini ni jambo linalofaa kutiliwa mkazo.

    Feri zote zinafaa kuwa na vyombo vya kuhakikisha usalama wa wasafiri na magari pia. Sheria mpya zinafaa kubuniwa ili kuwe na mpangilio katika feri hizi. Hakuna mtu ambaye anafaa kupoteza maisha yake kupitia kisa cha kuhuzunisha kama hiki.

    Picha kwa hisani ya: citizentv.co.ke

  • MWANARIADHA ELIUD KIPCHOGE  AMEWEKA REKODI DUNIANI

    MWANARIADHA ELIUD KIPCHOGE AMEWEKA REKODI DUNIANI

    Na Wangu Kanuri
    kanuriwangu@gmail.com

    Picha kwa hisani ya: Reuters

    Oktoba 12 mwaka wa 2019 ni siku ambayo daima itakuwa kumbukumbu kwani mwanariadha Eliud Kipchoge amevunja rekodi aliyokuwa amejiwekea ya kukimbia kwa kilomita arubaini na mbili kwa muda wa saa moja na dakika hamsini na tisa.

    Isitoshe jina lake limeandikwa katika kitabu cha rekodi cha dunia cha Guiness. Eliud aliyekuwa amejibidisha na kuamini kuwa ataweka historia duniani, aliwafanya wakenya wengi kujumuika kumtizama akivunja rekodi hii iliyofahamika kama INEOS 159.

    Rais Kenyatta aliwaongoza wakenya katika kumhimiza Kipchoge kulenga lengo lake huku naibu wake mheshimiwa Ruto na bibiye wakisafiri Vienna kumpa mkono anapokimbia.

    Kusudio kuu lake Kipchoge lilikuwa kuonyesha kuwa hakuna pingamizi lolote iwapo mtu anataka kuwa wa kwanza katika lolote. Isitoshe, alisisitiza kuwa hashindani na wengine bali anashindana na muda na kuweka historia katika dunia.

    Shindano hili liliokuwa likitizamwa moja kwa moja katika mitandao, limewafunza watu kuwa; shindano letu si dhidi ya marafiki, maadui ama wenzetu bali dhidi ya muda. Pili, mbio yetu yapaswa kuwa dhidi ya lengo tulizojiwekea na mwishowe mbio yetu ni katika tunayonuia kulenga.

    Eliud Kipchoge vilevile amesema kuwa alikuwa mwenye tumbo joto baada ya kupokea simu kadha wa kadha kutoka viongozi wakuu katika serikali ya Kenya ikiwemo rais Kenyatta. Hata hivyo, bado alishikilia msimamo wake dhidi ya kuweka rekodi ya wanariadha duniani.

    Akizungumza baada ya shindano hilo, Kipchoge amesema kuwa imemchukua mwanadamu miaka sitini na tano kuweka historia katika mbio za dunia kwa hivyo yeye amejazwa na furaha ghaya kuweza kuifufua historia hii. Mwenyekiti wa INEOS bwana Jim Ratcliffe alisema kuwa hakuamini vile Kipchoge alikimbia mtawalia mbio ya kwanza kwa muda wa chini ya saa moja.

    Picha kwa hisani ya: New York Post
  • DAYSTAR HEALTH AWARNESS WEEK

    DAYSTAR HEALTH AWARNESS WEEK

    The Daystar Compassion and Care Centre (DCCC) Health Awareness week which took place this October as from 7th to the 10th saw many students and staff show up to get tested for free.

    The Health Awareness week is a norm that takes place every once a semester for a week at Athi River and Nairobi campus. They take place around the same time in both campuses.

    For the Athi River campus, DCCC outsourced health practitioners from The Nairobi Women’s Hospital, Kitengela branch. Students showed up in numbers to get tested and know their health status.

    There were different stalls for different health departments including; optical, dental, general physician, height and weight, BMI, pressure and sugar/ diabetes. HIV/AIDS testing and counseling was also available for students.

    A law in Kenya was passed to make testing and counselling for HIV a private matter and a personal decision. Therefore the stall for HIV testing had to be secluded in a private space where nobody could eavesdrop or see the counselor or the patient. It took place in the DCCC offices.

    Students turned up in large numbers to test for HIV after the seclusion on the testing center. This is due to the fact that the testing center was secluded and therefore the privacy encouraged students to get tested.

    This was a strategic move by DCCC since over the years the HIV testing has always been done in the open and most of the time students did not show up due to fear and embarrassment.

    A student heading for check up at the tents


    Click here to find photos from the health awareness week and DC3 chapel

  • PHOTO STORY: DC3 HEALTH WEEK AND CHAPEL

    PHOTO STORY: DC3 HEALTH WEEK AND CHAPEL

    From 7th to 11th October Daystar Compassion and Care Centre, hosted health week in Athi River Campus.

    Find photos from the health week and the DC3 chapel below.

    Photos courtesy of: Joseph Gichari

    Josephndungo55@gmail.com

    Click here to read about the Health Awareness week

  • ETHIOPIAN PRIME MINISTER WINS THE NOBEL PEACE PRIZE FOR HIS BORDER PEACE DEAL WITH ERITREA

    ETHIOPIAN PRIME MINISTER WINS THE NOBEL PEACE PRIZE FOR HIS BORDER PEACE DEAL WITH ERITREA

    By: Valyne Laibuta

    vklaibuta@gmail.com

    Thumbnail image courtesy of: The Telegraph

    Prime Minister of Ethiopia Abiy Ahmed. Photo courtesy of: KTVQ.com

    Ethiopian Prime Minister, Abiy Ahmed won the Nobel Peace Prize on Friday for mending relations with Eritrea, Ethiopia’s long-standing rival.

    Abiy was deserving of this award “in particular, for his decisive initiative to resolve the border conflict neighboring Eritrea” said Brett Reiss-Anderson, Chair of the Nobel committee, who decides which individual is deserving of the phenomenal award. 

    According to the Washington Post, the peace deal between Abiy and his Eritrean counterpart, Isaias Afwerki, formally ended a 20-year-old military standoff that led to Eritrea’s secession in 1993. 100,000 people lost their lives in the standoff that occurred between 1998-2003. The border dispute erupted into a full-blown war between the two neighboring nations.

    Not only has he been able to mend ties with Eritrea, but the 43-year-old former intelligence officer has ushered a new era of peace and hope in Ethiopia that was riddled with authoritarian regimes. In this new era he has:

    • Released thousands of political prisoners
    • Lifted bans of various political organizations
    • Prosecuted former officials accused of torture
    • Vowed to move Ethiopia into its first free, multi-party elections in 2020

    Abiy Ahmed is the third sitting head of government from Africa that has won the lucrative award. Previous African heads of states that have won the Nobel Peace Prize are Ellen Johnson-Sirleaf, former president of Liberia and F.W. de Klerk who won it jointly with Nelson Mandela in 1993 as South Africa transitioned from apartheid. 

    Last year the award was awarded jointly to 64-year-old Dennis Mukwege, a Congolese doctor who treated thousands of women who had been raped or sexually assaulted as a result of conflict in Congo, and 26-year-old Nadia Murad, who advocated for the support and freeing of Yazidi women who had captured and held as sex slaves by the Islamic State (IS).