Category: Jamvi la Kiswahili

  • TABIA NCHI

    TABIA NCHI

    {Picha kwa hisani ya As You Know}

                                                   

    Na: Gertrude Prosper

    {getrude2003@gmail.com}

    Tabianchi ni hali ya mabadiliko ya mazingira ya hali ya hewa ikiwemo joto, mvua na pepo. Mabadiliko ya tabianchi yanapojitokeza kunaweza kutokea ongezeko la mawimbi ya joto, mizozo ya kimataifa, mafuriko na ukame unaoathiri viumbe hai.

    Kwa asilimia kubwa, mabadiliko haya yanachangiwa na shughuli za binadamu ikiwemo uchomaji wa makaa na mafuta katika viwanda, vituo vya umeme na kwenye magari.

    Ongezeko la joto linaweza kuleta athari kama vile; viwango vya maji baharini kupanda, bahari kuchemka na kuwa na tindikali zaidi, barafu vya vilele vya milima kuyeyuka na kusababisha mafuriko, kubadilika kwa mikondo ya bahari, ukosefu wa mvua itakayosababisha njaa na uhaba wa maji, ongezeko la halijoto, upepo, tufani na kuenea kwa magonjwa. Zaidi ya hayo, madhara haya yanaweza kusababisha vifo vya watu na viumbe hai kama mimea na wanyama na kuvifanya kutoweka.

    Janga hili la ongezeko la joto linaweza kuepukika ikiwa watu watachukua hatua ya kupanda miti, kupunguza kiwango cha utoaji wa hewa chafu ya kaboni, kukabiliana na matatizo ya taka yanayojikusanya kwenye mito na kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi.

    Kando na hayo, watu wanaweza pia kujenga nyumba zinazoweza kumiliki mabadiliko ya tabianchi ili kuwa salama. Njia hizi ikiwemo kujenga kwa kuzingatia ukame, viwango vya joto, mafuriko, baridi, vimbunga na upepo mkali.

    Tunatakiwa kuhamisha uwekezaji wetu kutoka kwenye uchumi mchafu kuenda kwenye uchumi msafi unaotumia teknolojia inayowafikia watu wote katika nchi zote.

  •   BIASHARA YA OMBAOMBA

      BIASHARA YA OMBAOMBA

    {Picha kwa hisani ya Mwananchi}

     

    Na: Gertrude Prosper

    {getrude2003@gmail.com} 

    Tumekua tukiona watu ikiwemo watoto na wazee walemavu barabarani wakiombaomba ili waweze kujikimu kimaisha. Ila cha kushangaza ni kwamba wengi wao wapo kibiashara, na sio tu biashara ya kawaida ila ni ile ya kutumikishwa.

    Baadhi ya watu hawa wanageuza kuwa mtaji, na nyuma yao ni watu wenye uwezo wanaowatumia ili kunufaika na kufaidi hizo hela au msaada unaotolewa kwa watu hawa. Kisichoaminika ni kua pesa hizo hupitia hesabu ya hali ya juu kama tu mapato mengine. Walemavu wengi hulazimishwa kutimiza matakwa ya waajiri wao ingawa hawaipendi kazi hiyo, kwani “Lisilo budi hutendwa.” Wengine wao wanahadaiwa kua wanatajirika katika biashara hio lakini mwishowe wanateswa, kunyanyaswa na kulipwa kiasi kidogo kisichowatosha.

    Changamoto inatokea pale mtu anapotaka kuwasaidia watu hawa wasiojiweza, anashindwa kujua nia ya kweli ya watu hao wanaohitaji msaada, kumbe wapo hapo kwa kulazimishwa.

    Watoto walemavu pia wanalazimishwa kuomba mitaani na wasipoleta pesa hua wanapigwa. Familia nyingi zinadanganywa kuwatoa watoto wao na kuenda kufanyishwa biashara ya kikatili na haramu. Watoto hawa wanasafirishwa na kuletwa kuja kutumikishwa mbali na wazazi wao na kulamishwa kukatika mawasiliano na wao.

    Kwa watoto wanaotumikishwa, imegundulika kua chanzo ni malezi. Wazazi au walezi wanadanganywa watoe watoto walemavu na kupewa ahadi kua watapewa misaada ya kifedha kama malipo yao ilhali watoto hao wanaenda kuteswa. Wazazi na walezi hawa wanatakiwa kuzingatia malezi ya watoto wao walemavu na kuhakikisha hawakati  tamaa kwa watoto hao na badala yake kuwalinda ili kuepukana na mazingira hatarishi. Jamii pia inatakiwa kuhakikisha kwamba watoto hawa walemavu wanalindwa ili wawe raia wema na sio mzigo kwa Taifa. Sio watoto tu, hata wazee walemavu wanahitaji ulinzi kwa sababu wanyanyasaji hawa wananufaika wakijua watu hawa wenye ulemavu hawajiwezi na wengine wametelekezwa.

    Hata hivyo, mbali na hawa wasiojiweza kutumikishwa, kuna walemavu, wanaofanya ajira hii kwa hiari kutokana na hali yao ya maisha kua ngumu, na hio ndio njia pekee itakayowawezesha kuishi na kutunza familia zao kwa wale wenye watoto. Wamama wenye watoto walemmavu au wamama mlemavu wenye watoto na wameachwa na waume zao kutokana na hali yao, huteseka sana. Walemavu hawa wanakubali kutumiwa kama vitega uchumu ingawa ni kwa mateso, kwani kwao “heri nusu shari kuliko shari kamili”.

    Hali nyingine ni ya ombaomba tapeli, ambayo pia ni biashara inayofanywa na baadhi ya watu wanaojifanya walemavu wakiombaomba ilhali si walemavu bali ni matapeli. Watu hawa wameamua kuanza biashara hii kwani wanaamini kuwa watu huwasaidia au kuwapa fedha watu wenye ulemavu tu. Mwisho wa siku, utawaona watu hawa wakielekea nyumbani bila ulemavu wowote, baada ya kuvuna ambapo hawakupanda.

    Watu hawa utawaona wakitambaa barabarani wakiwa wamevaa mavazi yaliyochakaa kabisa ili watu wengine waamini kuwa hawajiwezi. Kuna baadhi yao pia hukodisha watoto wao au wa ndugu na kuwatumia kama kitega uchumu ili tu wahurumiwe na kuchangiwa pesa. Wengi wao hutumia usafiri wa bodaboda ili wasionekane au kujulikana na watu.

    Biashara hizi za ombomba ni kinyume na sheria kwani inawazuia watu wenye ulemavu kutopata msaada kwasababu ya uoga uliojawa watu ya kuwa wanatapeliwa. Wapita njia wengi na hata waendesha magari wamepunguza kiasi cha kuwasaidia ombaomba barabarani kwa sababu wengi wao hawana ulemavu na hawaaminiki.

    Serikali inatakiwa kuwasaidia walemavu hawa na kuwashika hao matapeli  wanaojifanya.

  •  MFANYAKAZI WA NYUMBANI

     MFANYAKAZI WA NYUMBANI

    {Picha kwa hisani ya Conde Nast Travelers}

     

    Na: Gertrude Prosper

    {getrude2003@gmail.com}

    Kwa miaka mingi sasa watu wengi wamezoea kuwaajiri wafanyakazi wa ndani ili kuwasaidia kazi. Wafanyakazi hawa wa nyumbani ni wasaidizi au wakelezaji wa kazi zote za nyumbani ikiwemo kufua, kupika, kufanya usafi wa nyumba na mazingira, kuosha vyombo na baadhi ya kazi zingine nyingi wanazopewa na waajiri wao. Mbali na kazi hizo, wafanya kazi wengi hupewa kazi ya kulea watoto endepo mama au wazazi ameenda kazini, au kama wanataka kuendelea na shughuli zingine.

    Kabla sijaelezea jinsi baadhi ya mambo ya ajabu ambayo wafanyakazi huwafanyia watoto, tutaanza na jinsi wafanyakazi hawa huteswa katika baadhi ya sehemu wanapoajiriwa. Kwanza kabisa, mtu anapomwajiri mfanya kazi anatakiwa ahakikishe kua hamtesi wala kumyanyasa kwa namna yoyote ile, na badala yake anatakiwa akumbuke haki yake. Hii ni kwasababu wafanyakazi hawa ndio walinzi wa nyumba na wana uwezo wa kuiangamiza au kuistawisha familia.

    Wafanyakazi hawa hupitia changamoto nyingi kama vile kunyimwa chakula na mavazi mazuri, kupigwa, kutopewa mahali pazuri pa kulala, kufanyishwa kazi nyingi nje ya uwezo wao na hata kubakwa au kunyanyaswa kijinsia na waajiri wao. Waajiri hawa husahau mchango mkubwa unaotolewa na wafanyakazi hawa ingawa bado wanawahitaji.

    Kumetokea kesi nyingi ya wafanyakazi hawa wa ndani wa kike, kubakwa au kunyanyaswa kijinsia na waajiri wao wakiume na hii imeleta migogoro katika familia nyingi na kusababisha kuvunjika kwa ndoa. Wengi wao wakitoa malalamiko, hawaaminiwi kwa sababu wanalaumiwa kuwa sababu ya kilichowapata. Unapata mume au baba mwenye nyumba ana familia ya pili na mfanya kazi wa ndani.

    Kuna baadhi ya haki ambazo wafanya kazi wanastahili kupewa ikiwemo likizo kwa sababu wengi wao hufanya kila siku bila kupumzika na inawalazimu kusingizia kuumwa ili waweze kupumzika au kuenda kuwasalimia wazazi wao nyumbani. Wanatakiwa pia walipwe mishahara yao kamili na kwa wakati, na kuhakikisha ulinzi wa afya na usalama wao.

    Kati ya hayo machache kuhusu haki na usalama wa wafanya kazi wa nyumbani, tutaangazia vitendo vya ajabu vinayofanywa na wafanyakazi hawa katika familia tofauti haswa kwa watoto wanaoachiwa kuwalea.

    Wafanya kazi hawa wa ndani hushikwa wakiwadhulumu, kushiriki kingono na watoto wa waajiri wao na wakati mwingine kuwapiga na kuwaumiza watoto hawa. Inasikitisha kwa sababu watoto hawa hushindwa kutoa mashtaka kwa wazazi kutokana na umri wao kua mdogo na sababu nyingine ni vitisho wanavyopewa. Wafanya kazi wengi hunyanyasa watoto kwa sababu ya kukosa subira pindi mtoto anapokataa kula, kulala au kumsikiliza.

    Wazazi hawa hugundua hizi shida na mateso watoto wao wanayoyapitia baadae sana wakati mtoto ashaharibiwa kupitiliza. Kesi nyingi zimetolewa dhidi ya wafanya kazi wa nyumbani lakini bado idadi inatia shaka. Wazazi wanatakiwa wahakikishe wanawaajiri wafanyakazi wazuri waliobobea ili watoto wao wawe kwenye mikono salama, kwa sababu wakati mwingi wapo kazini na wanachelewa kurudi hivyo hawajui kinachoendelea nyumbani. Wakati mwingine wazazi hawa wanashauriwa angalau kukaa na mtoto kwa muda mwingi na sio tu kutokomea kazini ilhali mtoto hayupo salama.

    Kutokana na uzoefu wa kuwaachia wafanya kazi wa nyumbani watoto ili wawalee, hamna namna nyingine bali kuhakikisha wafanya kazi hawa ni wa kuaminika na wenye utu na huruma.

     

  •    AFYA YA AKILI

       AFYA YA AKILI

    (Photo courtesy of uCheck Blog)

    Na: Gertrude Prosper

    getrude2003@gmail.com 

    Afya ya kiakili ni hali ya kuwa sawa kiakili, kisaikolojia na kuwa na mawazo chanya. Afya ya kiakili ni muhimu kwa sababu inahusiana na jinsi akili ya mtu inavyofanya kazi.

    Miaka inavyozidi kuenda, afya ya kiakili inaharibiwa na hivyo kusababisha watu kupata matatizo ya kiakili. Matatizo haya ya kiakili hayachagui jinsia, aina ya kazi mtu anayofanya wala umri, mtu yeyote anaweza kupata, sanasana vijana ndio wanaonekana kuathirka kwa asilimia kubwa. Watu wengi wamezoea kupuuzia kuhusu afya ya akili zao na hii imewafanya kugundua kua wanamatatizo ya kiafya baadae wakati wameshachelewa.

    Mwelekeo wa matatizo ya afya ya kiakili duniani unazidi kutia shaka kutokana na idadi ya watu inavyozidi kuongezeka. Wataalamu wa afya ya kiakili wanatakiwa waongeze bidii ili kutoa matibabu na huduma dhidi ya vyanzo vya matatizo ya akili. Sio waatalamu tu, hata ndugu, jamaa na marafiki wanaweza kuwa msaada mkubwa kwa watu hawa.

    Vyanzo au vichochezi vya matatizo ya kiakili ikiwemo ukatili wa kingono/ kijinsia, uonevu, unanyasaji, unyanyapaa, ubaguzi, ugumu wa maisha na ukiukaji wa haki za binadamu. Vyote hivi vinaweza kumsababishia mtu kupata matatizo ya afya ya kiakili. Kando na hayo, huzuni, kusononeka, hofu, woga na hasira ya kila wakati vanaweza kua ni vyanzo vya matatizo ya akili.

    Vyanzo wengine ni migogoro katika familia ikiwemo wazazi au walezi kugombana mbele ya watoto, kuwapiga watoto wao au kutumia lugha isiyofaa kwa watoto. Hii inaleta matatizo ya kisaikolojia kwa watoto. Wazazi au walezi wanatakiwa kua mifano bora kwa watoto kwasababu hawa ndio vijana watakaokuja kuteseka kiakili baadae. Wazazi wanatakiwa wahakikishe kuwa wao ndio mstari wa mbele kuwalinda na kuwajengea watoto mienendo na maadili inayofaa katika maisha. Vijana ndio taifa la kesho.

    Athari za kutoshughulikia matatizo ya afya ya kiakili husababisha mambo makubwa kama vile kuleta misongo ya mawazo, kiwewe, kuwalazimu watu kujiua na matumizi ya pombe na mihadarati.

    Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwepo kwa ripoti nyingi za mauaji kutokana matatizo ya kiakili, na bara la Afrika likiwa linaongoza kuliko mabara mengine duniani. Takriban zaidi ya watu 10 kati ya 100,000 hufa barani Afrika, ambayo ni zaidi ya wastani wa kimataifa. WHO imesema kuwa Afrika ina uhaba wa matibabu na huduma wa magonjwa ya afya ya kiakili, hii ni kutokana na imani potofu zinazowafanya watu kupuuzia magonjwa haya. Watu hawa wanapokosa msaada wanalazimika kujiua au kufanya matendo ya kujiumiza.

    Mtu anapoishi kwa huzuni mwingi, kukosa usingizi, kua na mshtuko, mawazo mabaya, upweke, dhiki, wasiwasi au kusikitika kushusu maisha, ni vizuri kutafuta msaada mapema kabla ya kufanya mambo ya kujiumiza.

    Matibabu ya kiakili na huduma ni pamoja na kuzungumza au kuwasiliana na watu unaowaamini ikiwemo marafiki, familia, wahudumu wa afya, na wakijamii. Mawasiliano kwa kawaida ni kwa ajjili ya kupashana au kubadilishana habari, hisia, maoni au mawazo kwa kutumia maneno, maandishi au ishara.  Watu wengi hushindwa kuwasilisha hisia zao kwa muda unaofaa na hii huwasababishia madhara mengi ikiwemo afya ya kiakili. Wengi wao huona ni vigumu kujielezea kwa wengine kutokana na aibu au kutotaka kuonekana wadhaifu. Utayari wa kuzungumza ili kutafuta suluhisho ni hatua muhimu sana, kwasababu inaweza kumsaidia mtu kuepuka kujiua au kupata misongo ya mawazo.

    Ni sawa kutokua sawa, hauko pekee yako. Tafuta msaada mapema.

  • MGENI KIPOFU

    MGENI KIPOFU

    (Picha kwa hisani ya MuseumNext)

     

    Na Abdul S. Shaban

     

    Tazama bila ya hofu, hapo ndipo utaona,
    Alosema muongofu, alitazama kwa kina,
    Pasinapo hitilafu, mimi naye naungana,
    Kuwa mgeni kipofu, hata kama anaona.

    Mgeni huwa kipofu, hata kama anaona,
    Vitu vyenye upotofu, hasemi atauchuna,
    Huwa anaudhohofu, mjuvi kuonekana,
    Kweli mgeni kipofu, hata kama anaona.

    Hata aone mnofu, nayo pilau imefana
    Huku njaa takatifu, mgeni imembana,
    Kusema ni ualifu, japo aona bayana,
    Haki mgeni kipofu, hata kama anaona.

    Mwisho ninawaarifu, wa juzi, leo na jana,
    Muone na msadifu, wala hamtabishana,
    Zaidi utamsifu, mjumbe wake Rabbana,
    Haki mgeni kipofu, hata kama anaona.

  • MAONYESHO YA NANENANE

    MAONYESHO YA NANENANE

    (Picha kwa hisani ya Tanzania Agricultural Development Bank)

     

    Na Gertrude Prosper

    Nane Nane ni likizo ya umma nchini Tanzania inayosheherekewa tarehe 8 Agosti, kila mwaka. Ni siku ya maonyesho ya kilimo ambapo wakulima wote nchini wanafanya maonyesho yao ya mazao, mifugo, dawa, na bidhaa katika kanda mbalimbali.

    Leo, Agosti 8 2022 ni kilele cha maonyesho ya nanenane ambapo viongozi pamoja na wananchi wanatembelea mabanda tofauti kujionea mbinu mbalimbali za kilimo bora, uvuvi na mifugo. Wajuzi, wajasiriamali na wataalamu wapo kuadhimisha siku hii kwa kuonyesha bidhaa zao na virutubisho mbalimabli vya mifugo mfano kuku, nyuki, nguruwe na ng’ombe. Wakulima pia wanauza bidhaa kama mashine, dawa, wanatoa elimu na bima ya mazao shambani.

    Siku hii ni muhimu kwasababu inawapa watu fursa ya kuonyesha teknolojia mpya na maendeleo katika kilimo, na kujua zaidi kuhusu uvuvi na ufugaji wa wanyama tofauti. Inawapa watu pia elimu, ujuzi na njia mbalimbali ya kufanya kilimo bora ili kupata mazao mengi ya chakula na biashara. Hii inaongeza vyakula nchini na mapato kwa kuuza nje katika nchi mbalimabli.

    Heri ya Sikukuu ya Nanenane

  • Penzi Halijaribiwi, Utanaswa Unasike.

    Penzi Halijaribiwi, Utanaswa Unasike.

    (Picha kwa hisani ya The Economic Times)

    Na Abdul Shaban

     

    Mapenzi ya siku hizi, ni ya nipe ndo nikupe,

    Tena ya tele mapozi, kadhalika na mapepe,

    Sipo jali tawa chizi, ujipake na matope,

    Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

     

     

    Penzi halina mjuzi,  nina kwambia peupe,

    panga yako mamuzi, mabaya uje utupe,

    ya sikutoke machozi, yakalovya zako hope,

    Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

     

     

    Mapenzi toka awali, yaliwashinda wa kale,

    Usijione mkali, utarudi na tandale,

    Samsoni nguvu kali, alinaswa palepale,

    Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

     

     

    Ukijifanya bahili, kutosikia wavyele,

    Utashikika pahali, upige zako kelele,

    Kusifiwa ni muhali, huwezi kusonga mbele,

    Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

     

     

    Kujipiga na kifua, eti wewe umakini,

    Utakuja kujutia, ushindwe na kibaini,

    Utalia na dunia, uhame nako nyumbani,

    Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

     

     

    Mwisho nikimalizia, kwa huu wangu waraka,

    Polepole kuanzia, sikuwa nayo haraka,

    Nadhani mumesikia, madada na kina kaka,

    Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

  • Nakusifia

    Nakusifia

    (Picha kwa hisani ya WBUR)

    Na Abdul Shaban

    Mke ninakusifia,
    Mzuri umetulia,
    Na wala sitojutia,
    Kifua nakitanua.

    Nakupongeza kwa hili,
    Nyumbani nikiwasili,
    Moyo wangu huwa tuli,
    Hali unanijulia.

    Nilipanga mikakakati,
    Masijidi nikaketi,
    Dua pia na swalati,
    Nikamuomba jalia.

    Nikataraji mazuri,
    Mwenye dini ndo mzuri,
    Mola akanitabiri,
    Wewe ndo ukanijia.

    Sitara unatimiza,
    Mazuri wanihimiza,
    Kikosea wanijuza,
    Toba nije kutubia.

    Wanihimiza kwakweli,
    Nichume yalo halali,
    Adhabu zake Jalali,
    Kwangu unanihofia.

    Hongera we mke wangu,
    Wanilelea wanangu,
    Malezi yaso machungu,
    Mola wao kumjua.

    Naomba kwake manani,
    Tusitengane ndoani,
    Wenye shari maishani,
    Wacheze pata potea.

    Zimekujaa swifati,
    Mahabuba habibati,
    Nitazimaliza beti,
    Sifa hazitoishia.

    Utenzi naumaliza,
    Machozi nabubujiza,
    Nikimuomba muweza,
    Amani kutujalia.

    Hapa sasa ndo kikomo,
    Hilo ndilo langu Somo,
    Sitoufunga mdomo,
    Nitazidi kusifia.

  • Pendo

    Pendo

    (Picha kwa hisani ya Adobe Stock)

    Na Abdul Shaban

    (abdoolmtyro@gmail.com)

     

    Ukipenda tafakari lako pendo,
    Unaempambania ana pendo?
    Au unapambana ili upate pendo?

     

    Nakupenda sikatai na wajua,
    Ila bado hunifai my dear,
    Hunipendi sikatai mi najua,
    Ila bado siamini mi nalia.

     

    Nalilia nini zaidi ya pendo?
    Kwako sina meno, mi siumi yani magego,
    Ninakupenda na sijapenda mpango wa kando,
    Hili sio pendo mi naapa hili ni tego.

     

    Hukunipa furaha hata nilipokufurahisha wewe,
    Ukaniacha kwa mataa nikizongwa na mwewe,
    Lako penzi nakataa bora nibaki mwenyewe.

     

    Zile chomoa chomeka humaliza chaji,
    Na hili betri likiisha hakuna wa kulichaji,
    Kutwa utalizungusha ufundi nao kipaji,
    Ghafla nalo lakufa ujione mkosaji.

     

    Kosa si kosa nakataaa,
    Kosa ni kosa hapo sawa,
    Kosa la kunichosha na kunitosa,
    Kosa la kukuposa ni langu na sitabisha.

  • Je, muda wa mshambuliaji wa Manchester United, Christiano Ronaldo, umekwisha Old Trafford?

    Je, muda wa mshambuliaji wa Manchester United, Christiano Ronaldo, umekwisha Old Trafford?

    (Picha kwa hisani ya News18)

    Na Abdul Shaban

    Manchester United ilitangaza siku ya Alhamisi jioni kwamba Cristiano Ronaldo hatakuwa nao watakaposafiri kwa ndege kwenda Bangkok Ijumaa kwa ajili ya mechi ya kwanza ya Erik ten Hag akiwa meneja.

     

    Ronaldo ameruhusiwa kusalia Ureno, kwa ruhusa ya United, kushughulikia suala la kifamilia ambalo halijawekwa bayana.

     

    Mchezaji huyo nmwenye umri wa miaka 37 , ikumbukwe, alipoteza mtoto wa kiume mnamo Aprili, wakati mpenzi wake alipojifungua pacha, mmoja tu ndiye alyenusurika.

     

    Hakuna kiasi cha pesa au umaarufu unaoweza kumkinga mtu kutokana na aina hiyo ya kiwewe.

     

    Hata hivyo habari hizo zilijiri siku tano baada ya hamu ya Ronaldo kutaka kuondoka United msimu huu wa kiangazi kuwa hadharani.

     

    Na ingawa hatakuwepo, hiyo itakuwa simulizi ambayo itatawala wakati wote ambapo klabu hiyo itakuwa nchini Thailand, na kisha Australia, ambako watacheza mechi ya Jumanne dhidi ya wapinzani wao wa zamani Liverpool.

     

    Saa moja kabla ya Ronaldo kubainika kwamba hatokuwa katika safari ya kuelekea Thailand , chanzo kimoja kinachoifahamu BBC Sport kilisema kuwa hakukuwa na nafasi ya mchezaji huyo kuwa katika safari hiyo.

     

    Hatua hiyo ilijiri kutokana na imani kwamba Ronaldo lazima alikuwa na mpango wa kuondoka kwasababu , iwapo hataondoka , kile kilichojiri Wikendi kisingefanyika.

     

    Chanzo chengine cha United pia kiliunga mkono hoja hiyo. Wao pia walikubaliana kwamba sakata hiyo itakwisha wakati Ronaldo atakapoondoka katika klabu hiyo alioyowasili kwa mbwembwe za aina yake Agosti iliopita , baada ya kujiunga huku klabu ya Manchester City pia ikiwa na hamu ya kumsajili.

     

    Kwa upande wao Man United inasema kwamba Ronaldo haendi popote , wakidai kwamba ana mwaka mmoja katika kandarasi yake kuondoka kitu kinachomfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi katika ligi ya premia na kwamba wanatarajia kwamba ataheshimu kandarasi hiyo.

     

    Hata hivyo klabu inapaswa kusema hivyo ili kulinda mali zao. Wanajua kuwa katika soka ni mara chache wachezaji wanashikiliwa na mikataba yao ikiwa wamedhamiria kuondoka, hakika si wachezaji wa hadhi ya juu kama Ronaldo.

     

    Wakati mwingine msimamo huo unaendelea kwa wiki – kama Bayern Munich wanavyofanya sasa na mshambuliaji Robert Lewandowski – lakini kawaida makubaliano hufanywa na mchezaji anapata anachotaka.

     

    Katika hali hii, ajabu ni kwamba haitokani na dhamira ya Ronaldo ya kuendelea kucheza kwa kiwango cha juu zaidi, na kwamba hali ingeweza kufikia kilele mapema zaidi. Baada ya yote, ilikuwa dhahiri United haingeweza kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa kipindi kirefu kabla ya msimu kufikia kilele chake.

     

    Msisimko wa mechi za kujiandaa kwa msimu mpya

    United wamezoea masuala kama haya kutawala safari zao za mechi za kujiandaa kabla ya msimu mpya.

     

    Miaka mitatu iliyopita, katika ziara yao ya mwisho, kabla ya Covid kuwazuia ghafla, mzozo ulitawaliwa na iwapo Paul Pogba aliyechukizwa angerudi kutoka Marekani kwa wakati ili ndege ielekee Perth. Alifanya hivyo – lakini Romelu Lukaku alidhihirisha hadharani kutoridhika kwake kwa kujielekeza kwenye vikao vya mazoezi ya baiskeli ili apone jeraha ambalo lilipungua mara tu alipoondoka kwenda Inter Milan.

     

    Hiyo ilikuwa ziara ya kwanza ya Ole Gunnar Solskjaer kama meneja wa United. Licha ya kupata uzoefu huo kama mchezaji. Ten Hag anakaribia kugundua ushabiki wa klabu hiyo huko Mashariki mwanzoni – na jina lake kuu halitakuwepo ili kuondoa tahadhari hiyo.

     

    Badala yake, Ten Hag atakapokabiliana na vyombo vya habari – pengine Jumapili – kwa mara ya kwanza tangu lipozinduliwa Old Trafford, atakuwa na maswali mengi ambayo huenda asiwe na majibu – yaani ni lini au ikiwa Ronaldo ataanza kushiriki mazoezi pamoja na wachezaji wenzake.

     

    Je, Ronaldo ndiye suluhu au tatizo?
    Kuna mawazo mawili kuhusu uwepo wa Ronaldo United

    La kwanza ni kwamba alikuwa mmoja wa wachezaji wawili pekee – kipa David de Gea ndiye mwingine – kuibuka kutoka kwa msimu mbaya uliopita bila sifa zao kuingia doa . Alifunga mabao 24, ikiwa ni pamoja na hat-trick mbili, na, bila yeye, United ingekuwa katika hali mbaya zaidi kuliko ile waliyoishia.

    Lakini kuna simulizi nyingine, kwamba Ronaldo alikuwa mmoja ya sababu kuu zilizoifanya klabu kumaliza pale ilipomaliza.

    Inasemekana mara nyingi Ronaldo hapandi juu uwanjani – mkakati uliowekwa na mkufunzi Ralf Rangnick aloitarajia kutekeleza katika klabu hiyo baada ya kutimuliwa kwa Solskjaer mnamo Novemba. Pia ndio mbinu ilioanzishwa na Ten Hag katika timu yake huko Ajax.

     

    Lakini je, uwepo wa Ronaldo ulikuwa mbaya pia?

    Alitofautiana na Harry Maguire kuhusu unahodha na, kwa kuzingatia hadhi ya Ronaldo, ni rahisi kufikiria angekuwa na maoni ya moja kwa moja kuhusu mambo mengine pia. Aliondoka uwanjani kwa kusuasua mara nyingi baada ya mechi, kwa hivyo anaweza kuwa anasema nini faraghani kutokana na hali mbaya ya jumla Old Trafford?

     

    Ni kweli Ronaldo akienda, United hawana nambari tisa – na hawajamtafuta.

     

    Lakini City wameshinda mataji mfululizo ya Ligi Kuu bila hata moja. Kiuhalisia, matarajio ya United ni ya chini sana na tayari wana idadi ya washambuliaji wa kimataifa wenye kasi ambao, labda, wanaweza kubadilishana. Kuwasili kwa Christian Eriksen kutaongeza ubunifu unaohitajika kwenye kikosi chao. Inatarajiwa kutakuwa na uimara zaidi katika safu ya kiungo hata kama harakati za kumtafuta Frenkie de Jong wa Barcelona zitashindwa kufanikiwa.

     

    Wiki chache zijazo zitakuwa muhimu kwa Hag Kumi.

     

    Anajua Ronaldo atakosekana mwanzoni mwa kipindi chake. Kwa uwezekano wote hatakuwepo kwa safari nzima.

     

    Jukumu la Ten Hag katikia eneo la mashariki na kwingineko ni kuandaa mpango ambao utafaa bila yeye. Msimu wa United unaweza kuutegemea.